Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi
(Mpanda Hospitali)

Madaktari Bingwa Wabobezi wa Watoto kutoka Hospitali ya Kanda Mbeya

Posted on: November 8th, 2023

 Madaktari Bingwa Wabobezi wa Watoto wachanga kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya

Mbeya waja mkoani Katavi kutoa mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo watoa huduma za afya kwa Watoto

Wachanga mkoani Katavi.

Akizungumzia ujio huo, Wakati alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi mapema leo Novemba

07, 2023, Dr. Lazaro Mboma, Ambaye ni Bingwa Mbobezi wa Upasuaji wa watoto kutoka Hospitali ya Rufaa

ya Kanda ya Mbeya, Amesema mafunzo hayo yatakuwa ya siku 3 na ni kwa Watoa huduma wote wa Mkoa wa Katavi.

Kwa upande mwingine, Dr. Mboma ameupongeza Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi kwa ubunifu wa

kutengeneza vitanda vya kulalia watoto wachanga {Baby Cots} huku akiahidi kuwa Hospitali ya Rufaa ya kanda

ya Mbeya itashirikiana kwa ukaribu katika mambo mbalimbali na Hospitali ya rufaa ya Katavi.