KAMBI MAALUMU YA MADAKTARI BINGWA - KATAVI RRH TAR: 11-15 SEPTEMBA 2023
Posted on: September 5th, 2023![](http://katavirrh.go.tz/storage/app/uploads/public/64f/c30/d28/thumb_277_800_420_0_0_crop.png)
Madaktari bingwa wa Hospitali ya Benjamini Mkapa kushirikiana na madaktari bingwa wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi watafanya kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu kwa magonjwa yafuatayo:
- Matibabu na uchunguzi wa magonjwa ya watoto ikiwemo moyo kwa watoto wenye viashiria.
- Kuona wagonjwa wenye matatizo ya mishipa ya fahamu. Upasuaji kwa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi
- Matatizo ya afya ya uzazi wajawazito wenye changamoto mbalimbali za uzazi
- Magonjwa ya mfumo wa chakula
- Wagonjwa wenye shida ya mfumo wa mkojo, nguvu za kiume na uzazi wa mwanaume
- Magonjwa ya mifupa, maumivu sugu ya magoti na nyonga
- Matatizo ya macho
- Kufanya upasuaji wa mifupa salama
- Matatizo ya masikio, Pua na Koo ikiwa ni pamoja na upasuaji wake.
- Kisukari, shinikizo la damu na kiharusi
- Uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya figo
Tunawaomba wananchi mjitokeze kwa wingi kuchunguza na kupata matibabu kwa utaratibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi kuanzia tarehe: 11 – 15/09/2023