Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi
(Mpanda Hospitali)

HUDUMA ZA UCHUJAJI DAMU ZAANZA RASMI KATAVI RRH

Posted on: February 24th, 2025

Huduma ya Uchujaji Damu {Dialysis) imeanza rasmi mwezi huu wa Februari 2025

katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi.


Akiongea katika Mahojiano yake na kituo cha Radio cha Mpanda FM, Mganga

Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi, Dr. Deogratias Banuba

amesema kuwa kuanza kwa huduma hiyo kutawasaidia sana wakazi wa Mkoa

wa Katavi na mikoa Jirani.


"Kipindi cha nyuma huduma hii ya Uchujaji Damu haikuwepo, Wakazi wa hapa Katavi iliwalazimu waende Hospitali za mikoa ya Mbeya, Dodoma na Mwanza ili waweze kupata huduma hii. Kwasasa tunawakaribisha watu wote wenye changamoto za Figo na ambao wameanza tayari kupatiwa matibabu haya katika Hospitali za mikoa ya mbali waje kwetu kwani tunatoa huduma kwa wateja wote wa BIMA na CASH" Dr. Banuba.


Huduma hii ya uchujaji Damu ni mpya na ya kwanza katika Mkoa wa Katavi,

Na ujio wa Huduma hii ni moja ya maboresho makubwa yanayofanyika

katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi.


Ujio wa huduma hii ya uchujaji Damu haitasaidia tuu Wakazi wa Mkoa wa Katavi,

Bali itasaidia pia wakazi wa mikoa Jirani na Mkoa wa Katavi.